VOICE OF CHANGE TANZANIA(V.O.C)
TAASISI YETU YA VOICE OF CHANGE
Taasisi yetu ya Voice Of Change (V.O.C) ni muungano wa watu shupavu na imara
kutoka pande zote za Tanzania wakiwa wahitimu wa fani mbalimbali
kutoka vyuo
vikuu, wanafunzi, wafanyakazi, wakulima,wafugaji ,na wenye kutoka katika sekta
mbalimbali wenye mzigo wa kuinua jamii kupitia vipaji vyao.Taasisi hii ya Sauti ya
mabadiliko ni taasisi ya kijamii, isiyo ya kisiasa,isiyo ya kiserikali,isiyo ya kidini,isiyo ya kidhehebu au
ya kibiashara inayojikita katika shughuli mbalimbali za kuisaidia jamii kupata
maarifa ya kibinadamu na kiutu ambayo inakusanya watu wenye mzigo na nia ya
kuleta mabadiliko kwa njia ya kupata elimu, ujuzi na maarifa yanayohusu masuala
mbalimbali ya kimwili,kitamaduni,kimaadili, kisaikolojia, kijamii, kiuchumi na
kiroho na hatimaye kuelimisha watu wengine kuleta mabadiliko katika familia
zao,maofisini,katika jamii inayowazunguka na taifa kwa ujumla .Taasisi hii pia inalenga
kuamsha vipaji ,vipawa ,uwezo na karama za watu kwa njia ya kuwafanya
wajitambue wenyewe ,wagundue hazina walizonazo ambazo hawatumii na baadaye
kuwaelekeza namna ya kuzitumia katika kusababisha kuleta maabadiliko na
maendeleo katika maisha yao na jamii inayowazunguka.
No comments:
Post a Comment